leo tutapata maujanja jinsi gani ya kurekebisha mac yako na kuirudisha kuwa safi (format) kwa internet.
njia hii ni njia nzuri sana na salama zaidi ya ku restore mac yako, njia hii itapunguza hekaheka njingi unazoweza kupata ukitumia njia nyingine ku restore.
utatakiwa kuwa na internet enye kwenda vizuri bila ku kata kata (stable) na pia uwe na bundle sio chini ya 5gb
JINSI YA KUANZA
Utawasha mac yako na kwa kutumia keyboard yako utabonya key 3 kwa pamoja ukiwa unawasha mac yako (option command + )
ukiwa umebonya izo key 3 kwa pamoja moja kwa moja utapelekwa kwenye recovery mode
utaendelea kufuata muongozo kutoka kwenye screen yako
apa utachagua wireless yako na kuweka password zako kama zipo
hatua hii ndipo umakini unapotakiwa zaidi kwa kuwa unataka ku restore mac yako na kuwa fresh kabisa kama mpya, utatakiwa kwanza uende kwenye disk utility ili ku format kabisa ndipo urudi kwenye re install os x, ukianza na reinstall osx moja kwa moja utaweza kupata errs zitakazokupa changamoto
Ndani ya disk utility utafuta data tayari kwa kuanza reinstallation ya os x
baada ya apa utarudi nyuma na kuendelea na installation na mac os x kwenye mashine yako, fuatiza tu miongozo inayotoka kwenye kioo mpaka unapimaliza kufanya restore mac yako.
mpaka hapo utakuwa ushamaliza ku restore mac yako na itakuwa safi kama mpya. enjoy
kama una swali tafathali comment apo chini
No comments:
Post a Comment